Simba Vs Azam: Mtakula za Kutosha!
ACHANA na mechi ya Man city na Spurs, ngoma leo saa 1 usiku iko kwenye Uwanja wa Taifa kwa Simba na azam. Kwa lugha rahisi ni kwamba wenye mpira wao Tanzania wanafungua msimu mpya kwa burudani ya Ngao ya Jamii. Kuanzia nje mpaka ndani ya Uwanja hizi ndizo klabu zenye bajeti kubwa zaidi na leo zinakutana Taifa kuonyeshana ubabe na kufungua njia mpya. Ni mechi ngumu na itakayokuwa na utamu wa aina yake. Ni lazima mtu akae, hakuna cha sare wala suluhu. Mtaalam Razack Abalora atasimama kwenye lango la Azam huku pembeni katika ulinzi wakisimama Nicholas Wadada na Bruce Kangwa. Pale kati atakuwepo Daniel Amoah na Oscar Masai. Kati yupo Yakub Mohammed, Abdallah Masoud, Salmin Hoza, Salum Aboubakary ‘Sure Boy’ na Idd Seleman. Huyu ni wakuitwa Nado. Pale mbele anamalizia Obrey Chirwa mwenyewe. Simba sasa. Aishi Manula hayuko fiti. Beno Kakolanya ataanza chini ya ulinzi wa Shomari Kapombe,Hussein Mohammed ‘Tshabalala’, Pascal Wawa na Tairone Dos Santos. Kuna mtu ...





Comments
Post a Comment