Posts

Showing posts from April, 2019

SIMBA SC YAIFANYIA UMAFIA YANGA SC

Image
IMBA imeingia kwenye anga za Yanga, baada ya kocha Patrick Aussems kumfukuzia beki anayewaniwa na vinara hao wa Ligi Kuu Bara. Wekundu wa Msimbazi, juzi Jumamosi walitupwa nje ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuchapwa 4-1 na TP Mazembe mjini Lubumbashi, na sasa hasira zao wanazihamishia kwenye Ligi Kuu Bara ili wapate nafasi nyingine ya kucheza Ligi ya Mabingwa mwakani. Tayari uongozi wa Simba umeshaanza mikakati ya kuwasaka wachezaji wakubwa ili wawe na nguvu zaidi msimu ujao wa Ligi ya Mabingwa, na wanataka wavuke hatua ya robo fainali ambayo wamekomea msimu huu. “Tumejifunza vitu vingi hadi hatua hii ambayo tumefikia na kutolewa. Tumeona kwamba ili usonge mbele kwenye hatua kubwa ni lazima uwe na wachezaji wenye viwango vikubwa na sisi kwa mwakani tutalifanyia kazi hilo,” alisema jana Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori. Kocha Patrick Aussems. Baada ya mechi hiyo ya ambayo ilichezwa huko Lubumbashi nchini DR Congo na Simba kufungwa mabao 4-1, kocha m

OKWI AWEKA REKODI YA DAKIKA 270 SIMBA

Image
SIMBA ilicheza kwa dakika 270 katika Ligi ya Mabingwa ugenini hatua ya makundi bila ya kufunga bao lolote kabla ya straika Emmanuel Okwi, juzi kufunga katika robo fainali na kuweka rekodi ya kipekee. Okwi ameweka rekodi ya kuwa mfungaji pekee wa Simba ugenini kwenye mechi za tangu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya timu hiyo kucheza dakika 270, sawa na mechi tatu bila kufunga bao lolote. Mganda huyo alifunga bao hilo mbele ya TP Mazembe katika mechi ya pili ya robo fainali ya kombe hilo ambapo Simba walifungwa kwa mabao 4-1 na kutolewa. Kabla Okwi hajafunga, hakukuwa na mchezaji mwingine wa Simba ambaye alifunga bao kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika ugenini tangu hatua ya makundi. Simba katika mechi zake za ugenini kuanzia hatua ya makundi, walicheza na Al Ahly wakafungwa 5-0, AS Vita 5-0 na JS Saoura 2-0.

AJIBU AONDOLEWA RASMI YANGA…KISA KIPO HAPA

Image
Ibrahim Ajibu HABARI za moto zinazosambaa kwa kasi kwenye ulimwengu wa michezo ni kuwa inadaiwa Klabu ya Yanga imeamua kuchukua maamuzi magumu na kumuondoa kikosini nahodha wake, Ibrahim Ajibu kutokana na kuwepo kwa taarifa kadhaa tata juu yake. Inaelezwa kuwa sababu kubwa ya kuchukuliwa kwa maamuzi hayo ni kudaiwa kuwa kuna ‘mgomo baridi’ ambao staa huyo amekuwa akiufanya kiasi cha kuhusishwa kuwa ni njia ya yeye kushinikiza aongezewe mkataba. Takribani wiki tatu sasa, Ajibu amekuwa nje ya kikosi hicho ikielezwa kuwa amekuwa akisumbuliwa na majeraha, jambo ambalo limekuwa gumu kuaminika kwa mashabiki na baadhi ya viongozi wa Yanga wakiamini kuna sababu nyuma ya kukosekana kwake uwanjani. Chanzo cha habari kimelieleza gazeti hili hivi: “Tayari viongozi wetu wameshamshtukia Ajibu juu ya janja yake ya kugoma kuisaidia timu katika michezo inayoendelea ili ashinikize kupewa mkataba mpya kwa kiwango anachotaka yeye, la sivyo aachwe na aende kuitumikia Simba msimu ujao. “H

YANGA WAPEWA SH BILIONI MOJA KUTOKA MAREKANI, NA UINGEREZA

Image
UNAWEZA kusema rasmi kamati ya uhamasishaji wa kuichangia Yanga, iliyozinduliwa Aprili 6, mwaka huu ndani ya Morena Hoteli mjini Dodoma, ambayo iko chini ya Naibu Waziri, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Anthony Mavunde, imeeleweka ambapo Watanzania waishio nchi za Marekani, Dubai na Uingereza wameichangia Sh bilioni moja. Michango hiyo inajumuisha Watanzania wanaotoka katika nchi nane maarufu kama Diaspora ambazo kwa pamoja zimeunda group la WhatsApp na kuipokea kwa kishindo kampeni hiyo, kiasi cha kuhamasishana mara moja na kuanza michango ambayo hadi sasa inadaiwa kukusanya zaidi ya kiasi hicho. Katibu wa Kamati ya Uchangiaji ya Yanga, mhandisi Deo Mutta, alisema mara baada ya kuizindua rasmi kampeni hiyo, Jumatatu iliyopita aliunganishwa katika group la Watanzania hao na kumpatia mikakati yao huku wakiomba akaunti rasmi watakayotuma fedha za mchango wao. “Kwa makadirio ya haraka hadi sasa hivi nimeona takribani dola mia tano na zaidi zimeshachangwa kupit

TAIFA STARS VS SENEGAL, ALGERIA AFCON, MAKUNDI YAPO HAPA

Image
TIMU ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, imepangwa Kundi C Kwenye michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (Afcon 2019) inayotarajiwa kuanza Juni 21 hadi Julai 19, mwaka huu. Droo ya makundi hayo ilichezeshwa jana usiku katika Mji wa Giza uliopo nchini Misri ambapo michuano hiyo ya 32 kwa mwaka huu inafanyika nchini humo. Katika kundi hilo, Taifa Stars imepangwa na Senegal, Algeria na Kenya, ambapo kwa mujibu wa ratiba ya Shirikisho la Soka Afrika (Caf), Taifa Stars itaanza kucheza dhidi ya Senegal, kisha Algeria na kumaliza na Kenya. Hii ni mara ya pili kwa Taifa Stars kushiriki michuano hiyo, mara ya kwanza ilikuwa 1980 ambapo ilipangwa na timu za Guinea, Morocco na wenyeji Nigeria. Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia na Kocha wa Taifa Stars, Emmanuel Amunike, walikuwa miongoni mwa wageni waalikwa walioshuhudia tukio hilo la kupangwa makundi.

MAN CITY YAPIGWA NA SPURS UGENINI BAO 1-0

Image
TOTTENHAM Hotspur wakiwa kwenye uwanja wao mpya wa London, jana walifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Man City kwenye kwenye mchezo wa kwanza wa robo fainali wa Ligi ya Mabingwa Ulaya. Awali wengi waliamini kuwa Man City wana nafasi kubwa ya kushinda mchezo huu lakini mambo yakawa magumu kwao na kujikuta wakifungwa bao pekee katika dakika ya 78. Katika mchezo huo ambao kila timu ilitawala kwa wakati wake, Son alikuwa shujaa baada ya kuifungia Spurs bao hilo muhimu na likiwa ni la kwanza kwao la Ligi ya Mabingwa Ulaya kwenye uwanja wao mpya. City walipata penalti ya utata mwanzoni tu mwa mchezo huo, lakini mshambuliaji wake Sergio kun Aguero shuti lake likapanguliwa na kipa wa Spurs, Hugo Lloris. Mwamuzi wa mchezo huo ilibidi atumie VAR kufahamu kama ni penalti au la baada ya Danny Rose kuunawa mpira kwenye eneo la hatari. Hata hivyo, baada ya penalti hiyo bado timu zote ziliendelea kushambuliana kwa zamu huku City wakikosa nafasi nyingi za wazi. T

ZAHERA AHOFIA UBINGWA KWENDA SIMBA

Image
Mwinyi Zahera YANGA kwa sasa wamebakisha mechi nane tu wamalize ligi msimu huu wa 2018/19, lakini kocha mkuu wa timu hiyo, Mwinyi Zahera amechungulia mbali na kuweka bayana kwamba viporo vya Simba vinamtisha kwani wakishinda vyote timu yake haitaambulia kitu. Kwa sasa Yanga ndiyo wameendelea kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi wakiwa na pointi zao 71 wakiwa wamecheza mechi 30. Wakati Yanga wamecheza mechi hizo Simba wenyewe wanakamata nafasi ya tatu katika ligi wakiwa na pointi 57 baada ya mechi ya mechi 22. Simba wao wamebakisha mechi 16 kabla ya kumaliza ligi. Kocha huyo raia wa DR Congo amefunguka kuwa anatishwa na hali hiyo kwa sababu mechi hizo 16 ni nyingi kulinganisha na zao nane. “Hizi mechi 16 ni nyingi sana kwa Simba, ni sawa kabisa na nusu ya michezo ya ligi ambayo timu zinatakiwa zicheze, mimi sikuona sababu hadi sasa timu inakuwa na mechi nyingi namna hii. “Hali hii inaweza kusababisha matatizo kwetu kama ikitokea kwamba wakashinda mechi zote. Kushind

SIMBA KUWATOA KWAO TP MAZEMBE KAMA WAANGOLA

Image
KWA kiwango na takwimu za uwanjani walizoonyesha Simba jana dhidi ya TP Mazembe uwezekano upo wa kufuzu nusu fainali. Katika mechi hiyo ya kwanza ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba ilitawala kwenye umiliki wa mpira, pasi na kila kitu kama inavyoonekana kwenye jedwali. Lakini ukiachana na takwimu hizo, Mazembe waliingiwa hofu na matokeo hayo kutokana na takwimu za msimu uliopita ambapo walitoka suluhu na Agosto nchini Angola lakini wakaenda kutoa sare ya bao 1-1 Lubumbashi na kutolewa. Katika mechi ya jana, Mohammed Tshabalala wa Simba na Jackson Muleka wa Mazembe ndiyo wachezaji pekee walionyeshwa kadi za njano hadi kipindi cha kwanza kinamalizika. Tshabalala alimchezea vibaya Sissoko wakati Muleka alidanganya kuanguka ndani ya eneo la penalti katika mchezo huo ambao Paschal Wawa alitolewa dakika tatu za kwanza baada ya kuchezewa rafu na nafasi yake kuchukuliwa na Juuko Murshid. Simba walifanya shambulio moja kali la dakika ya 31 Kagere alipiga mpi