Posts

Showing posts from July, 2018

HABARI ZA KITAIFASALUM KIHIMBWA AONGEZA MKATABA MTIBWA SUGAR

Image
KLABUya Mtibwa Sugar Sports Club imefanikiwa kuingia mkataba mpya na kiungo mshambuliaji wake Salum Ramadhani Kihimbwa. Salum Kihimbwa alikuwa amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake na sasa ameongeza miaka miwili hivyo Salum Ramadhani Kihimbwa mkataba wake na Mtibwa Sugar ni wa miaka mitatu na unatarajia kufikia tamati 2021. Akizungumza leo mjini Dar es Salaam, Katibu Msaidizi  wa Mtibwa Sugar, Abubakar Swabur juu ya mkataba wa Kihimbwa amesema wameboresha mkataba wa awali na hivyo ataendelea kuitumikia Mtibwa kwa misimu mitatu zaidi na hii ilitokana na kiwango chake katika msimu wa kwanza “Tumefikia makubaliano na Salum Kihimbwa ya kuongeza miaka miwili na alikuwa amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wa awali hivyo mkataba huu  ni wa miaka mitatu na utafikia kikomo 2021, ni furaha kwetu kwa kwakuwa tumemuongeza mkataba mtu sahihi kutokana na kipaji kikubwa alichonacho” Abubakar Swabur. Salum Ramadhani Kihimbwa alijiunga na Mtibwa Sugar akitokea Polisi Morogoro inayochez

NIYONZIMA kuchukuliwa hatua za kinidhamu?

Image
KAIMU Rais wa klabu ya Simba SC ya Dar es Salaam, Salim Abdallah ‘Try Again’ amesema kwamba kiungo Mnyarwanda Haruna Niyonzima atachukuliwa hatua za kinidhamu kwa kuchelewa kurejea nchini kujiunga na timu baada ya ruhusa maalum aliyopewa kuisha.

HABARI ZA KITAIFAHIZI NDIYO TAARIFA ZA MKWASA KUJIUZULU YANGA, SABABU NI…

Image
Inaelezwa kuwa Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa anatarajiwa kukabidhi barua ya kuachia madaraka hayo klabuni hapo sababu ikidaiwa kuwa ni za kiafya. Mkwasa aliyeanza kuitumikia Yanga kama mchezaji miaka ya 1980 kisha baadaye kuwa kocha amesema ameshauriwa hospitali kupata mapumziko. Mkwasa ambaye ni mume wa mwandishi wa habari na mtangazaji wa zamani wa Redio na Televisheni nchini, Betty Chalamila Mkwasa aliyeng’ara RTD na baadaye Redio One na ITV, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya wa zamani amekuwa kimya kwa siku kadhaa za hivi karibuni.

BAADA YA UFARANSA KUBEBA UBINGWA WA WORLD CUP, KOCHA WA MESSI AONDOLEWA KAZINI

Image
Muda mfupi baada ya Ufaransa kuhitimisha michuano ya Kombe la Dunia kwa kutwaa ubingwa, upande wa pili Shirikisho la Soka la Argentina (AFA), wamekubaliana na Kocha Jorge Sampaoli kufikia tamati ya mkataba wao. Sampaoli anaondoka Argentina baada ya kikosi chake kuboronga katika michuano ya Kombe la Dunia. Imeelezwa pande zote mbili zimeelewana. Pia Kocha wa viungo na Kocha wa mafunzo ya video nao wameachia ngazi. Sampaoli alikiongoza kikosi cha Argentina katika michuano hiyo mpaka hatua ya 16 bora na kutolewa nje na Ufaransa kwa kipigo cha mabao 4-3.

SAFARI YA EDEN HAZARD KWENDA REAL MADRID IMEKOLEA

Image
Mshambuliaji wa Chelsea, Eden Hazard anasema: "Pengine ni wakati wa kujaribu mambo tofauti baada ya miaka 6 ya kuvutia Stamford Bridge.” Kiungo huo mwenye miaka 27, aliyeihakikishia Ubelgiji ushindi dhidi ya Uingereza kwa kufunga bao la pili, waliposhinda 2-0 mechi ya kuwania nafasi ya tatu Kombe la Dunia, amehusishwa na kuhamia Real Madrid. "Mnajua ni wapi natamani kutua," Hazard aliwaambia waandishi Jumamosi na kuongeza: "Ninaweza kuamua iwapo nitaondoka au nitasalia lakini uamuzi wa mwisho ni wa klabu ya Chelsea - iwapo wanataka niondoke." Hazard ambaye anatajwa kuwaniwa kwa ukaribu na Real Madrid, ameishauri Chelsea kufanya usajili wa maana kabla ya msimu kuanza. Chelsea ilimpiga kalamu meneja wake Antonio Conte Ijumaa na kumnasa raia mwenzake wa Italia Maurizio Sarri, chini ya saa 24