Posts

Showing posts from February, 2018

CHIRWA ABAKI DAR KWENYE MECHI YAO NA SHELISHELI

Image
Kikosi cha Yanga kimeondoka asubuhi ya leo jijini Dar es Salaam kwenda Shelishli kwa ajili ya mchezo wa marudiano hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Saint Louis Suns utakaofanyika Jumatano mjini humo. Safari hiyo imekuja huku mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chirwa akilazimika kubaki Dar kutokana na kuwa majeruhi.  Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten amesema Chirwa pamoja na kiungo Thabani Kamusoko na mshambuliaji Donald Ngoma hawajasafiri kutokana na kutokuwa fiti kiafya. Wachezaji wengine majeruhi ambao nao hawajasafiri ni beki Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na mshambuliaji Mrundi Amissi Tambwe. Kikosi cha kamili cha Yanga kilichopondoka leo asubuhi ni: Makipa: Ramadhani Kabwili, Beno Kakolanya na Youthe Rostand. Mabeki: Hassan Kessy, Juma Abdul, Mwinyi Mngwali, Gardiel Michael, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Patto Ngonyani na Kelvin Yondani. Viungo: Said Juma ‘Makapu’, Papy Kabamba Tshishimbi, Pius Buswita, Raphael Daud, Yussuf Mhilu, Ibrahim Ajib, Said Mussa, E

KIKOSI CHA SIMBA -DJIBOUT KWA AJILI YA MCHEZO WAO NA GENDARMERIE KESHOKUTWA JUMANNE

Image
Kikosi cha Simba kimeondoka jioni ya leo kwenda nchini Djibout kwa ajili ya mchezo wao wa pili dhidi ya Gendarmerie Nationale, keshokutwa Jumanne. Kikosi kilichosafiri leo kuelekea Djibout ni:-  (1) Aishi Salum Manula (2) Emanuel Elias Mseja (3) Mohamed Hussein Mohamed (4) Mzamiru Yassin Said (5) Bukaba Paul Bundala (6) Emmanuel Arnold Okwi (7) Moses Peter Kitandu (8)Shiza Ramadhani Yahya (9) Nicholas Gyan (10) Erasto Edward Nyoni (11) James Agyekum Kotei (12) Shomari Salum Kapombe (13) Mwinyi Kazimoto Mwitula (14) Jonas Gellard Mkude (15) John Raphael Bocco (16) Ally Shomary Sharifu (17) Said Hamisi Juma (18) Yusufu Seleman Mlipili (19) Murushid Juuko (20) Kwasi Asante

KAMA KAWA HAJI MANARA HAWEZI KUWAACHA YANGA HIVIHIVI

Image
Simba na Yanga zipo nje ya mipaka ya Tanzania kwa ajili ya michezo yao ya kimataifa iliyopo chini ya Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), lakini huku nyuma hawajaondoka hivihivi. Kama kawaida yake Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara ametumia ukurasa wake wa Instagram kuwafanyia utani wapinzani wao wa jadi, Yanga kutokana na kuondoka nchini wakiwa wamevaa kaptura huku mmoja wa wachezaji wa Yanga akionekana ameshusha kaptura yake kwa chini kwa staili maarufu ya ‘kata K’. Manara aliweka picha ambayo inawaonyesha wachezaji wa Yanga wakiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kisha akaandika ujumbe huu: “Tofauti ya jumlisha na Msalaba...Tofauti ya Tende na Mende, malizia na tofauti ya Jua na Mvua......kupanga ni kuchagua......”  Baada ya hapo akaandika: “Loooh hizi kata K zingine bana! Boxer nje nje...ila ndiyo ukimataifa huo au siyo! Swap uone tofauti yao na yetu...au sisi tunapendelewa hivi vifaa?🤔🙇” Aidha, Manara aliamua kuweka picha

YANGA KUKWAMA KIMATAIFA,SIMBA KUPETA SHIRIKISHO

BOCCO NDIYE MSHAMBULIAJI BORA TANZANIA

Image
Simba imeendea kuwa na mwendelezo mzuri katika msimu huu wa 2017/18, ambapo inaongoza Ligi Kuu ya Vodacom na imeanza kwa kishindo katika Kombe la Shirikisho Afrika, lakini nyuma ya pazia kuna wachezaji ambao wamekuwa wakionyesha uwezo wa juu. Kuna wachezaji kadhaa wa timu hiyo ambao wameonyesha ni msaada wa Simba kwa safari hii, baadhi yao ni Emmanuel Okwi na Asante Kwasi, lakini kuna mtu anaitwa John Bocco huyu amekuwa akiwakosha mashabiki wengi wa Msimbazi kwa kasi yake ya kutupia. Mchambuzi wa masuala ya soka nchini Tanzania, Edo Kumwembe amemzungumzia mshambuliaji huyo wa Simba, John Bocco kwa kusema kuwa ndiye mshambuliaji bora kuliko wote kwa sasa nchini Tanzania kwa wazawa. Edo amesema hayo alipokuwa akichambua michezo leo asubuhi katika kituo cha Radio cha EFM ambapo alisema Bocco anastahili sifa hizo kwa kile ambacho amekuwa akikionyesha. “Ukiondoa kina Mbwana Samatta na Simon Msuva ambao wapo nje ya Tanzania, kwa sasa Bocco ndiye mchezaji bora kwa washambuliaji wa T

MZEE MWINYI ATENGUA KAULI YA TANZANIA NI KICHWA CHA MWENDAWAZIMU

Image
Baada ya kupita miaka mingi, hatimaye, rais mstaafu wa awamu ya pili ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Hassan Mwinyi ametengua kauli yake juu ya soka la Tanzania. Mzee Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi wa mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika (Caf), kati ya Simba dhidi ya Gendarmerie ulioshuhudiwa Simba ikipata ushindi wa mabao 4-0. Mzee Mwinyi alivutiwa na soka la Simba lililoonyeshwa kwenye mchezo huo na baada ya mechi alifuta kauli yake aliyoitoa miaka 30 iliyopita aliposema “Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu” . Akizungumza baada ya mchezo huo wa jana uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Mzee Mwinyi alisema:  “Nimeshuhudia mchezo mzuri na sasa nafuta lile neno kwamba Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kila anaetaka kujifunza kunyoa atunyoe sisi, sasa nyie ndio vinyozi.”

WALICHOKISEMA AZAM KUHUSU OKWI NA JONAS MKUDE

WACHEZAJI WA GHANA WAWEKA REKODI MECHI YA SIMBA DHIDI YA AZAM FC

Image
Mchezo wa Simba dhidi ya Azam FC uliopigwa jana kwenye Uwanja wa Taifa bado ni gumzo. Mtanange huo wa Ligi Kuu ya Vodacom ulimalizika kwa Simba kupata ushindi wa bao 1-0 mfungaji akiwa ni Emmanuel Okwi. Pamoja na ushindi huo, kulikuwa na gumzo lingine la wachezaji raia wa Ghana kutawal katika wachezaji walioingia uwanjani. Jumla ya wachezaji nane raia wa Ghana walicheza mchezo huo, idadi kubwa ya wachezaji wa kigeni kucheza kwa pamoja katika mchezo mmoja. James Kotei na Asante Kwasi walianza katika kikosi cha kwanza cha Simba huku Razak Abarola, Daniel Amoa, Yakubu Mohamed na Enock Atta-Agyei walikuwa kwenye timu iliyoanza kwa upande wa Azam. Baadaye Azam FC walifanya mabadiliko kwa kumuingiza Bernard Arthur (raia wa Ghana) kuchukua nafasi ya Yahya Zayd na Simba walimtoa Okwi nafasi yake ikachukuliwa na Nicholas Gyan (raia wa Ghana)  ambao walikamilisha idadi ya waghana nane kucheza mechi hiyo. Kwa sheria na kanuni za soka, zinaruhusu timu kucheza mechi ikiwa na wachezaj

VIDEO | HAJI MANARA: NIYONZIMA ANASEPA KWENDA INDIA Harun Habari Za Kitaifa 08 February 2018

SALAMU ZA PONGEZI KMC, AFRICAN LYON

Image
 Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kinazipongeza timu za JKT Tanzania, KMC na African Lyon  kwa kufanikiwa kuwa miongoni mwa timu sita zilizopanda ligi kuu daraja (VODACOM Premier League) kwa msimu wa 2018/19.  DRFA inaamini mafanikio waliyopata timu za JKT, KMC na African Lyon yametokana na uongozi bora pamoja na mipango mizuri waliyojiwekea katika vilabu vyao. Kwahakika wameutendea HAKI Mkoa wa Dar es Salaam.  Chama Cha Mpira wa Miguu mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kinawahakikishia vilabu hivyo vilivyopanda na vilabu vingine vilivyopo katika ligi kuu (VODACOM Premier League) kuwa DRFA itaendeleza ushirikiano uliopo na uongozi wake pamoja na kamati nzima ya utendaji ya vilabu hivyo katika masuala mbalimbali ya kuendeleza soka la Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla.  Kwa niaba ya kamati ya utendaji ya DRFA na familia ya mpira wa Miguu katika mkoa wa Dar es Salaam tunawapa pongezi za dhati kwa mafanikio hayo mliyoyapata na kuomba kuitumia nafasi hiyo kuweza k

AFYA YA EMMANUEL OKWI KABLA YA MCHEZO WA AZAM FC HAYA HAPA…

Image
Siku moja kabla ya kuivaa Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom, kuna taarifa nzuri kwa mashabiki wa Klabu ya Simba. Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi cha timu yake ambacho kitacheza mchezo wa kesho Jumatano dhidi ya Azam FC baada ya kuwa na hofu kuwa atakosekana. Okwi alishindwa kuendelea na mchezo wa timu yake dhidi ya Ruvu Shootingi katika kipindi cha kwanza baada ya kuumizwa shingoni na Mau Bofu wa Ruvu. Daktari wa Simba, Yassin Gembe amesema kuwa mchezjai wakeyuko fiti na hakupata majeraha makubwa, hivyo yupo kambini pamoja na wenzake kwa ajili ya mchezo huo.

YANGA 4-0 NJOMBE MJI UWANJA WA UHURU

Image
FULL TIME Mwamuzi anamaliza mchezo, Yanga inapata ushindi wa mabao 4-0. Dakika ya 93: Mchezo unaweza kumalizika muda wowote kuanzia sasa. Dakika ya 90: Zinaonyeshwa dakika 3 za nyongeza. Dakika ya 88: Chirwa anatoka nje, anaingia chipukizi Said. Dakika ya 88: Mashabiki wa Yanga wanaongeza nguvu ya kushangilia. Chirwa anaipatia Yanga bao la nne, anamalizia pasi nzuri ya Akilimali. Dakika ya 87: GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO Dakika ya 83: Akilimali wa Yanga anaingia, anatoka Emmanuel Martine. Dakika ya 82: Njombe wamepunguza kasi. Dakika ya 80: Yanga wanapata kona. Mahadhi anapiga inaokolewa. Dakika ya 75: Yanga wanapata kona, inapigwa inaokolewa. Dakika ya 73: Njombe wanajaribu kupambana kupata nafasi ya kusawazisha. Yanga wanapata bao la tatu, mfungaji ni Emmanuel Martine Dakika ya 68: GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO Dakika ya 67: Yanga wanaongeza kasi ya kushambulia. Dakika ya 64: GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO Yanga wanapata penati baada ya beki wa Njombe Mj

MANENO YA KOCHA WA SINGIDA UNITED

Image
Licha ya kufanikiwa kuiwezesha timu yake kusonga mbele katika michuano ya Kombe la Shirikisho, bado Kocha Mkuu wa Singida United, Hans van Der Pluijm amewatolea ‘povu’ Green Warriors. Kocha huyo ambaye ni raia wa Uholanzi amesema kuwa Green ambao ndiyo waliocheza nao katika mchezo huo wa Hatua ya 32 Bora, walitumia mbinu ya kujilinda na kucheza rafu nyingi kwa wachezaji wake kiasi kilichochangia wasiweze kupata ushindi walipocheza nao. Singida United walicheza dhidi ya Green Warriors kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar ambapo Singida walishinda kwa penati 4-3 baada ya matokeo ya sare katika dakika 90 za kawaida. Kocha huyo wa zamani wa Yanga amelalamika kuwa Green hawakucheza soka la kuelewa, huku akidai kuwa walikuwa wakitumia nguvu kubwa na zikachangia kupoteza burdani ya mchezo huo. Amesema anashukuru kuona timu yake imepata ushindi katika mchezo huo lakini kinacho muuma ni mbinu za wapinzani wao hao ambao waliwatoa Simba katika hatua ya nyuma kwenye mic

SIKIA HABARI YA OKWI?

Image
Baada ya kuendelea kuwasha moto kwenye Ligi Kuu ya Vodacom, mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi, ameelezea juu ya mipango yake katika ngazi ya kimataifa akiwa na kikosi chake hicho cha Simba. Okwi ambaye ni raia wa Uganda ameeleza kuwa anajipanga kuhamishia mabao yake katika michuano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Afrika. Ifahamike kuwa hadi sasa Okwi ameshafunga mabao 12 katika ligi kuu ya msimu huu na kuchangia Simba kuwa kileleni kwa muda mrefu.  Akizungumza wakati wa mazoezi ya Simba yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar, Okwi alisema anaamini akifunga mabao mengi timu yake itakuwa na nafasi nzuri ya kufanya vizuri na kuiwezesha kusonga mbele. Okwi amesisitiza kuwa michuano ya kimataifa ni muhimu na mchezo wao dhidi ya wapinzani wao kutoka nchini Djibouti  utakuwa mwanzo wa wao kufanya vizuri ngazi ya kimataifa. Katika orodha ya wafungaji wa ligi kuu, Okwi anaongoza akiwa na mabao 12 akifuatiwa na Obrey Chirwa wa Yanga ambaye yupo sawa na John Bocco w

YALIYOANDIKWA KATIKA MAGAZETI YA MICHEZO JANA

Image

MFARANSA WA SIMBA AZUNGUMZIA POINTI 7..................

Image
Kocha Mkuu wa Simba, Pierre Lechantre amesema utofauti wa pointi tano dhidi ya Azam FC na saba dhidi ya Yanga hautakiwiki kuchukuliwa kama sehemu ya timu yake kujihakikishia ubingwa badala yake kuna kazi kubwa inakuja mbele yao. Simba inaongoza katika Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2017/18 ikiwa na pointi 35 ikifuatiwa na Azam FC yenye pointi 30 kisha Yanga ikiwa na pointi 28. Lechantre amesema ushindani anaouona kwenye ligi ya Tanzania ni mgumu na amewataka wachezaji wake kuhakikisha kila mmoja anatekeleza majukumu yake ili kutimiza lengo lao la ubingwa. "Kuwa pointi saba mbele ya wapinzani wetu haijalishi sana kama ndiyo tumemaliza kazi, kwa aina ya ushindani ambao nimeuona, naamini kila mmoja anahitaji kujituma na na kutimiza majukumu yake," alisema Lechantre ambaye ni raia wa Ufaransa.