Posts

Showing posts from July, 2019

Taifa Stars yajipa kazi ya kushinda Kenya

Image
 TIMU ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, jana Jumapili ilishindwa kuutumia vyema uwanja wa nyumbani baada ya kutoka sare ya bila kufungana na Kenya katika mchezo wa kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (Chan). Mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ulishuhudiwa na mashabiki wachache waliojitokeza uwanjani hapo. Stars ililisakama lango la Kenya kwa muda mrefu na kipindi cha kwanza kilimalizika wakiwa wanaongoza umiliki kwa 60/40 lakini hawakuweza kuwa na makali ya kufunga bao. Stars ilipata nafasi tatu za wazi katika kipindi cha kwanza lakini ilishindwa kuzitumia vizuri kupata bao. Kipindi cha pili, Stars walifanya mabadiliko kwa kumtoa Ayoub Lyanga na kumuingiza Ibrahim Ajibu dakika ya 54, pia walimtoa Hassan Dilunga wakamuingiza Kelvin John dakika ya 66 lakini hawakuweza kubadili kitu. Dakika ya 84 Stars walifanya mabadiliko tena kwa kumtoa John Bocco na kumuingiza Salim Aiyee lakini bado hawakuweza kuip