Posts

Showing posts from May, 2019

FEI TOTO AJIKABIDHI AZAM FC

Image
KIUNGO tegemeo wa Yanga, Feisal Salum ‘ Fei Toto’ , amejikabidhi rasmi Azam FC, baada ya kusema klabu hiyo imekuwa ikimwinda kwa muda mrefu na kwamba yupo tayari kutua kama wataafi kiana na Yanga wanaommiliki kwa sasa. Fei Toto alijiunga na Yanga msimu uliopita kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Singida United, ambapo tangu atue klabuni hapo, amekuwa ni mmoja wa wachezaji wenye mvuto mkubwa kwa mashabiki wake, hivyo kama ikitokea akachukuliwa na Azam, ataacha simanzi nzito kwao. Akizungumza na Championi Ijumaa, Fei Toto alisema ni kweli Azam wamekuwa wakimfuatilia muda mrefu hivyo kwa kuwa msimu huu unaelekea ukingoni, yeye yupo tayari kutua Azam ikiwa watatimiza vigezo na masharti ya uhamisho kutoka Yanga. “Sina tatizo la kujiunga na Azam maana wamekuwa wakinifuatilia kwa muda mrefu, lakini mbali na hilo mimi kama mchezaji siwezi kuchagua timu ya kuchezea, zaidi naangalia maisha yangu hasa kwa sasa ambapo umri wangu bado ni sahihi kutafuta maisha bora,” alisema. Ch

SIRI YA POGBA KUHAMA YAFICHUKA

Image
Paul Pogba WAKALA Mino Raiola imebainika ndio chanzo cha Paul Pogba cha kutaka kuondoka Manchester United. Staa wa zamani wa Tottenham na timu ya Taifa ya Misri, Ahmed Hossam `Mido’ alisema anafahamu kuwa wakala Raiola ndio anamvuruga Pogba kiasi cha kushikilia kutaka kuondoka msimu huu. Mido, ambaye alifanya kazi na Raiola kwa kipindi cha miaka 10, alisema anafahamu kuwa Raiola atakuwa bize akisaka timu ya kumnunua Pogba. Manchester United haina mpango wa kumuuza kiungo huyo ingawa kumekuwa na taarifa kuwa Pogba mwenyewe anashinikiza aondoke. Real Madrid kwa muda mrefu sasa inahusishwa kama timu ambayo inataka kumsajili Pogba na Mido amefichua kuwa wakala huyo atakuwa anafanya mambo yake chini kwa chini. “Wakala wa Pogba ni Mino Raiola na mimi nimefanya kazi na Mino, ambaye alikuwa wakala wangu kwa miaka 10 kwa hiyo nafahamu vizuri namna anavyofanya kazi,” alisema Mido. Mido alisema kuwa Raiola atakuwa ameshapiga hesabu zake na kuamini sasa ni wakati muafaka wa

Coastal Union kuikazia Simba leo

Image
KOCHA wa Coastal Union, Juma Mgunda amesema kuwa wamejipanga kupata matokeo chanya kwenye mchezo wao wa leo dhidi ya Simba utakaochezwa Uwanja wa Uhuru. Coastal Union wana kumbukumbu ya kupoteza mchezo wao wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Mkwakwani kwa kufungwa mabao 2-1 hali iliyowafanya wapoteze pointi tatu wakiwa nyumbani. Akizungumza na Championi Jumatano, Mgunda alisema; “Ninaitambua Simba ni timu kubwa na wana wachezaji wenye uzefu ila hilo hainipi taabu kwa kuwa ni timu inayofungika na mbinu zao tayari nimeshazijua.” “Nimewapa kazi ngumu mabeki kuzuia kasi ya mashambulizi ya Simba na pia nimewapa kazi ngumu washambuliaji kuliandama lango la mpinzani lengo ni kupata pointi tatu, mashabiki sapoti ni muhimu,” alisema Mgunda. Coastal Union imecheza jumla ya michezo 33 ipo nafasi ya 10 ikiwa na pointi zao 41 huku Simba ikiwa nafasi ya pili baada ya kucheza michezo 30 ina pointi 78.

ALIYEITUNGUA SIMBA AKARIBIA KUTUA YANGA SC

Image
UNAMKUMBUKA yule winga matata aliyemchambua beki wa Simba, Zana Coulibaly na kutupia? anaitwa Hassan Kabunda wa KMC, unaambiwa anakaribia kutua Yanga. Kabunda alimchambua Coulibaly na kufunga bao la kusawazisha katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza ambao ulimalizika kwa Simba kushinda mabao 2-1. Katika mchezo huo, tofauti na bao hilo winga huyo mwenye kasi alionekana mwiba katika kutokana na kiwango alichokionyesha. Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumatano, tayari Yanga imeanza kufanya mazungumzo ya awali na winga huyo aliyewahi kuwaniwa na Simba. “Muda mrefu kocha Mwinyi Zahera amekuwa akiomba mawinga wawili wa kushoto na kulia wenye uwezo mkubwa wa kupiga krosi na kasi wakiwa ndani ya uwanja. “Katika mahitaji yake hayo Kabunda ni mmoja wa wachezaji ambao amewataja na viongozi wameridhishwa na uwezo wao wa ndani ya uwanja na kikubwa kinachokwamisha hivi sasa ni suala la fedha. “Hivyo, kama mambo yatakwenda

AMUNIKE ATANGAZA CHA STARS AFCON

Image
Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kilichotangazwa na Kocha Emmanuel Amunike kwa ajili ya mashindano ya AFCON na CHAN.

STRAIKA MKENYA MAMBO SAFI YANGA

Image
DIRISHA la usajili likifunguliwa, Yanga huenda ikafanya kazi moja tu kutangaza orodha ya kikosi chake na watakapopiga kambi. Kama mambo yakienda sawa huenda kabla ya Ligi haijamalizika wakatangaza kabisa wanaoachwa bila kupepesa macho. Kocha Mwinyi Zahera amemalizana na kiungo mshambuliaji wa Kati wa Kariobang Sharks ya Kenya, Duke Abuya. Mchezaji huyo mwenye umbo kubwa na machachari amemwaga wino kwenye mkataba wa miaka miwili mbele ya Mwinyi Zahera. Abuya aliichapa Yanga mabao mawili katika mchezo wa robo fainali ya Mashindano ya SportPesa ambapo Wakenya hao walishinda mabao 3-2 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Januari 22, mwaka huu. Chanzo makini kutoka ndani ya Yanga kimeeleza kuwa, tayari kocha wao Mwinyi Zahera ameshamalizana na kiungo huyo na kilichobaki ni kutua nchini kwa ajili ya kutambulishwa rasmi kwa mashabiki. “Kocha ameshamalizana na kiungo mshambuliaji wa Kariobang Sharks ya Kenya, Duke Abuya ambaye ameingia mkataba wa miaka miwili na kwamb