Posts

ANZA MWAKA 2019 VIZURI KWA KUBEBA MAMILIONI KIRAHISI NA SOKABET

Image
HII ndiyo Januari ya mwaka 2019, huu ndiyo wakati sahihi wa kufanya maamuzi ya maisha yako kujua ramani itakuwaje kwa mwaka wote huu. Unachotakiwa ni kujiwekea akiba, upande wa pili Sokabet ambayo ni kampuni inayojihusisha na mchezo wa kubashiri matokeo ambayo huduma zake ni za kiwango cha juu tofauti, inaweza kukutimizia sehemu ya mipango yako kwa kushiriki kwa kiwango kidogo tu cha fedha. Sokabet inakuwezesha kubashiri matokeo kupitia tovuti ya  www.sokabet.co.tz  pia unaweza kufanya hivyo kwa kutumia simu yako ya mkononi ambapo unaweza kupata hadi Sh milioni 100 kwa kubet. ANZA KUSHIRIKI SASA Kama bado haujajiandikisha, unaweza kufanya hivyo leo kwa kuingia www.sokabet.co.tz bonyeza ‘SIGN UP’, jaza nafasi chache zilizo wazi, ukimaliza utatumiwa namba yako ya siri kwa njia ya SMS. Rejea sehemu iliyoandikwa ‘LOGIN’, andika namba yako ya simu, ingiza namba ya siri uliyotumiwa kwa SMS, hapo utakuwa umeshaingia kwenye akaunti yako rasmi. Utakaporejea baa...

KISA SIMBA, WAARABU WAVUTA JEMBE LINGINE

Image
BAADA ya kumsainisha mshambuliaji Mtanzania, Thomas Ulimwengu, Klabu ya JS Saoura ya Algeria, imevuta jembe lingine tayari kwa kuwakabili Simba Jumamosi ijayo kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika. JS Saoura itapambana na Simba kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi wa michuano hiyo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar. Kundi D pia lina timu za Al Ahly ya Misri na AS Vita ya DR Congo. Sasa kwa mujibu wa taarifa kutoka Algeria ni kwamba JS Saoura imemsajili mshambuliaji, Rafik Boukbouka aliyetokea Klabu ya Us Beni Douala ya Algeria ambayo ipo ligi ya madaraja ya chini kwa mkataba wa miaka mitatu. Saoura imemsajili Boukbouka baada ya kuvutiwa na kasi yake ya utupiaji mabao ambapo mpaka anaondoka Us Beni Douala, alikuwa Ibrahim Mussa, Dar es Salaam BAADA ya kumsainisha mshambuliaji Mtanzania, Thomas Ulimwengu, Klabu ya JS Saoura ya Algeria, imevuta jembe lingine tayari kwa kuwakabili Simba Jumamosi ijayo kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika. JS Saoura itapambana na Simba kwenye mchezo...

KISA SIMBA… KOCHA AS VITA AMPIGIA SIMU ZAHERA

Image
MUDA mfupi tu baada kuona amepangwa kundi moja na Simba SC kwenye  Ligi ya Mabingwa Afrika, Kocha Mkuu wa AS Vita Club ya DR Congo, Florente Ibengé,  fasta akainua simu na kumpigia Kocha wa Yanga,  Mwinyi Zahera. AS Vita ambayo ipo mjini Kinshasa, DR Congo, imepangwa kundi moja na Simba kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Timu zingine zilizopo kwenye kundi la la D ni  Al Ahly ya Misri na JS Saoura ya Algeria. Simba itaanza karata yake kwa kucheza na JS Saoura anayochezea Mtanzania Thomas Ulimwengu, Jumamosi ijayo na mechi ya kwanza dhidi ya  AS Vita  itakuwa Januari 19, kule  DR Congo  na watarudiana jijini Dar, Machi 15, mwaka huu. Kama hujui ni kwamba Kocha Ibenge ndiye bosi wa Zahera pale kwenye Timu ya Taifa ya DR Congo, yaani Ibenge ni kocha mkuu na Zahera ni msaidizi wake. Akizungumza na Championi Jumamosi, Zahera ambaye huu ni msimu wake wa kwanza kuinoa Yanga, alisema kuwa mara baada ya Caf kupanga makundi hayo a...

ISHU YA YONDANI, UONGOZI YANGA WAKUBALIANA NA ZAHERA

Image
UONGOZI wa Yanga umemaliza Sakata lililojitokeza hivi karibuni kati ya kocha mkuu wa timu hiyo raia wa DR Congo, Mwinyi Zahera na aliyekuwa nahodha wao, Kelvin Yondani. Sakata hilo ni lile la Zahera kumvua Yondani unahodha wa timu hiyo na kumkabidhi majukumu hayo, Ibrahim Ajibu kutokana na kile alichodai kuwa ni kuchoshwa na vitendo vya utovu wa nidhamu vya beki hiyo. Uamuzi wake huo ulionekana kutoungwa mkono na baadhi ya watu ambao waliona kuwa Zahera hakumtendea haki Yondani, lakini baada ya mvutano wa hapa na pele juu ya sakata hilo hatimaye uongozi wa Yanga umekubaliana na maamuzi hayo ya kocha wao huyo. Habari za kuaminika kutoka ndani ya Yanga ambazo  Championi Jumatatu  limezipata zimedai kuwa, baada ya uongozi huo kupokea ripoti ya Zahera kuhusiana na mabadiliko hayo, umekubaliana na jambo hilo. “Uongozi umehitimisha sakata hilo baada ya kukubaliana na maamuzi ya Zahera dhidi ya Yondani kwani baada ya kuipitia ripoti yake, umekubaliana na maamuzi ha...

WACHEZAJI YANGA WAMPINGA MWINYI ZAHERA

Image
Mwinyi Zahera MUDA mfupi baada ya wachezaji wa Yanga kumaliza mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar, kocha wa timu hiyo, Mwinyi Zahera akatangaza kumvua unahodha beki Kelvin Yondani jambo lililowashangaza baadhi ya nyota wa kikosi hicho. Yondani alikabidhiwa kitambaa cha unahodha mkuu na aliyekuwa beki nguli kikosini humo, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ambaye alistaafu miezi michache iliyopita na sasa ni meneja wa timu hiyo. Zahera ambaye amekuwa hataki utani linapokuja suala la nidhamu, ameweka wazi kuwa amemvua Yondani kitambaa hicho na kumkabidhi mshambuliaji mwenye kipaji, Ibrahim Ajibu. Chanzo cha Zahera kumvua unahodha Yondani ni kutokana na utoro mazoezini ambapo alichelewa kuripoti baada ya muda waliopewa wa mapumziko ya siku tano kupita na hakutoa taarifa yoyote. Zahera alisema: “Kuanzia leo (jana) mimi kama kocha wa Yanga nimeamua kumtoa unahodha Kelvin Yondani na atabaki kuwa mchezaji wa kawaida kama wachezaji wengine. “Nilitoa siku tano ...

KOCHA SIMBA AHOFIA UZOEFU CAF

Image
Patrick Aussems KOCHA Mkuu wa Simba, Mbelgiji, Patrick Aussems amefunguka kuwa kundi lao katika Ligi ya Mabingwa Afrika lipo wazi kutokana na kila timu kuwa nafasi ya kufanya vizuri lakini hofu kubwa ni kikosi chake kukosa uzoefu. Simba imepangwa Kundi D ikiwa na Klabu ya Al Ahly ya Misri, AS Vita Club yaDR Congo na JS Saoura ya Algeria na itaanza kutupa karata yao Jumamosi ijayo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar. Aussems ameliambia Championi Jumamosi kuwa, kundi lao lipo wazi kwa kila timu kuweza kufanya vizuri kutokana na timu watakazocheza nazo lakini anapata wasiwasi juu ya wachezaji wake kukosa uzoefu wa muda mrefu kwenye michuano hiyo kama ilivyo kwa wapinzani wao. “Binafsi naona kundi letu lipo wazi, linatoa nafasi kwa timu zote kuweza kufanya vizuri kwa sababu ukiangalia AS Vita wamecheza fainali ya Kombe la Shirikisho msimu uliopita kama ilivyo kwa Al Ahly katika Ligi ya Mabingwa Afrika. “Lakini hofu yangu ipo kwenye upande wa uzoefu kwa kuwa hawa wanacheza ...

‘MO SALAH ANAPOTEZA MUDA LIVER’

Image
IMEELEZWA kuwa Mohamed Salah ‘Mo Salah’ atakuwa tayari kuondoka Liverpool ikiwa vigogo wa Hispania, Barcelona au Real Madrid watamfuata kwa nia ya kumsajili Hayo ni maoni ya mshambuliaji wa zamani wa Tottenham na Misri, Mido ambaye ameweka wazi kuwa anaamini Liverpool haitakuwa na nguvu ya kumzuia ikiwa vigogo hao wataamua kumsajili. Mo Salah amekuwa katika kiwango kizuri kwa misimu miwili, msimu huu ameifanya timu yake iwe moja ya zinazowania ubingwa katika Premier League. Hadi sasa Salah, 26, amefunga mabao 16 katika michezo 27 ya michuano yote akiiongoza Liverpool kuongoza kwenye msimamo wa Premier pamoja na kufuzu hatua ya mtoano katika Ligi ya Mabingwa Ulaya. Akizungumzia uwezo wa raia mwenzake huyo wa Misri, Mido, 35, alisema: “Huwezi kujua litakalotokea kwenye soka. Barcelona au Real Madrid zikikutaka lazima kichwa kichemke, mchezaji yeyote yupo hivyo.” Akaongeza kuwa ikiwa msimu huu pia atafikisha mabao 25 anaamini vigogo hao watamfuata kwa nia ya kumsajili. “Nafiki...